Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema asema Rais akiendelea kufikiri yeye ni Mungu basi Mungu atasitisha maisha yake kabla ya 2020.

Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema akihutubia wakazi wa kata ya Sombetini alikuwa akifafanua juu ya kilichotokea baada ya mzozo wake na Mkuu wa Mkoa Mrisho Gambo na hatua ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kumpongeza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha Mbunge huyo katika Video niliyoambatanisha hapa amesema kuwa "Kitu kimoja ambacho rais anafikiri yeye ni Mungu na kwasababu amefikiri yeye ni Mungu, basi Mungu atasitisha maisha yake kabla ya Uchaguzi wa 2020".

Lakini Mwanzo wa hotuba yake alianza kwa kuimba wimbo wa "Majanga" wa msanii Snura Mushi kuelezea ugomvi wake na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Mashaka Gambo.