Tatizo la Chunusi na Namna ya Kulikabili soma hapa upate maarifa za kukufanya uonekane mpya kila siku


Chunusi ni jambo la kawaida wakati wa balehe na
zinatokea kwa sababu Mvulana au msichana
anafikia hatua ya muhimu ya maisha ya kutoka
utotoni kwenda katika utu uzima.




Wakati wa
balehe, tezi za ngozi zinazozalisha mafuta
mafuta yanayolainisha ngozi hutenda kazi zake
kwa uchangamfu mkubwa na kuzalisha mafuta ya
ngozi yaitwayo ‘sebum’.


Kazi ya sebum ni kulainisha ngozi kwa msichana
na kuleta mwonekano wa kisichana unaopendeza
na kuvutia.


Sebum inapozalishwa kwa wingi
inasababisha vinyweleo katika ngozi vizibe na
kuleta tatizo la chunusi.


Chunusi zikiwa nyingi
sana zinatazamwa kama ugonjwa wa ngozi na
hili linaweza kuwa tatizo la kurithi.

Ikiwa wazazi
au ndugu walikuwa na chunusi nyingi, kuna
uwezekano mkubwa wewe pia kupata chunusi
kwa wingi.


Hofu, woga na wasiwasi pia vinaweza kuchangia
msichana kupata chunusi. Hii huwatokea
wasichana wengi wanaopata hofu wakati wa
mitihani au muda mfupi baada ya hedhi.


Licha ya
ukweli kuwa mahangaiko ya kihisia husababisha
chunusi, tatizo la chunusi pia husababisha tatizo
la mahangaiko ya kihisia kwa wasichana wengi
wanao hangaikia urembo na uzuri wa ngozi ya
usoni.


Wasichana wengi wanaopata tatizo la chunusi
hawafurahii kile wanachokiona katika kioo
wanapojipodoa, lakini ukweli ni kwamba chunusi
hazitoshi kuwa chanzo cha kumpotezea
msichana raha na furaha katika maisha yake.


Pale chunusi zinapokuwa tatizo la kihisia,
msichana hana budi kushughulikia tatizo hili kwa
namna ambayo inadumisha afya ya mwili na akili
zake.



Jinsi ya Kukabiliana na Tatizo:


1. Safisha uso kwa maji na sabuni kila siku jioni
na asubuhi.


Fanya hivyo pia unapomaliza kufanya mazoezi au
unapotokwa na jasho.

Msichana yeyote asikubali
kulala usiku bila kusafisha uso au kuoga. Hii
itasaidia kuondoa mafuta kwenye ngozi na
kupunguza bakteria wanaoshambulia na
kusababisha uvimbe wa chunusi.


2. Usikamue chunusi ambazo hazijaiva, pia
usizishikeshike ili kuepuka makovu meusi usoni
na hatari ya kupata uvimbe wa uso pamoja na
ugonjwa hatari wa ubongo (cavernous sinus
thrombosis).


Mtu akipata ugonjwa wa ubongo unaotokana na
kukamua chunusi, anaweza kupoteza maisha
kama hakupata matibabu ya haraka na ya
uhakika na katika hali kama hii mtu mwenye
imani za kishirikina anaweza kufikiri kuwa
amerogwa.


3. Msichana mwenye tatizo la chunusi imempasa
kuepuka kutumia vipodozi vyenye mafuta na
vichocheo vya steroidi hasa katika sehemu zenye
kuathiriwa na chunusi.


Nywele zisafishwe kila siku

na mitindo ya nywele inayosababisha nywele
kugusana na ngozi ya usoni au mgongo iepukwe.


4. Pata nafasi na muda wa kukaa kwenye
mwanga wa jua kila siku hasa wakati wa asubuhi
ili sehemu zenye chunusi zipate mwanga wa jua
kwa muda wa wastani.

Mwanga wa jua unasaidia
kuimarisha afya ya ngozi na kuuwa bakteria
wanaosababisha chunusi kuvimba.


Tahadhari ichukuliwe kuhusiana na jambo hili
kwani kukaa kwenye mwanga wa jua kwa muda
mrefu hasababisha ngozi kuzalisha mafuta kwa
wingi na kuongeza tatizo la chunusi.



Jambo hili
pia linaweza kusababisha saratani ya ngozi,
kuzeeka kwa ngozi mapema au ngozi kuwa na
mikunjo na kukaukiana.




5. Kula vyakula vyenye asili ya mimea, matunda,
nafaka na mboga za majani husaidia mwili
kupambana na tatizo hili.


Kunywa juisi ya karoti
glasi moja kutwa mara tatu kila baada ya saa 8
kwa kipindi cha mwezi mmoja, husaidia katika
udhibiti wa chunusi.

Unaweza pia kupaka usoni
karoti zilizopondwapondwa na kuziacha zikae
usoni kwa zaidi ya dakika 20 kila siku kabla ya
kuziondoa kwa kunawa maji.


Karoti zina vitamini
A inayosaidia ngozi ili isipate makovu meusi
yatokanayo na chunusi.


Kunywa maji mengi kila
siku na hakikisha pia unapata mapumziko na
usingizi wa kutosha kila siku.


6. Epuka matumazi ya dawa za uzazi wa mpango
zenye vichocheo vya ujinsia kama vile vidonge
na sindano.

Tumia dawa za kusafisha ngozi kama
vile ‘benzoyl peroxide cleanser, anza na 2.5%, 5%
na hatimae 10%, kusafisha sehemu zote zenye
chunusi.


Hii husaidia kupunguza bakteria wanaoshambalia
chunusi juu ya ngozi na kuifanya ngozi iwe kavu
na kupunguza mafuta katika ngozi.

Kama chunusi
zinazidi hata baada ya kutumia tiba hiyo hapo
juu, onana na daktari kwa matibabu zaidi.