CHADEMA Wagoma Kuhamia Dodoma, Wadai Hawana Mpango Huo, ACT Wazalendo wao wanasemaje?

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema wazo la kuhamia Dodoma halimo kwenye ajenda zake.

Akizungumza na Mwananchi hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji alisema chama hicho hakina mpango wa kuhamia Dodoma kwa sababu hayo ni masuala ya kisiasa yasiyo na msingi kiuhalisia.

“Sisi makao yetu makuu yapo Dar es Salaam, hata katiba yetu ndivyo inavyosema, tutaendelea kuwa hapahapa. Hayo ni mambo ya kisiasa yasiyo na misingi ya kiuhalisia, hata mazingira hayaruhusu, kwa hiyo sisi tutaendelea kuwa hapa (Dar es Salaam),” alisema Dk Mashinji.

Chama cha ACT Wazalendo kilisema kuifanya Dodoma kuwa makao makuu ya nchi ni miongoni mwa ajenda zake.