OFISI ZA GAZETI LA TANZANIA DAIMA HAPAKALIKI WANADAIWA ,MMILIKI WA GAZETI HILO ADAIWA KUWA MBOWE


Taarifa zilizonifikia hivi punde ni kuwa Tanzania Daima wako kwenye crisis kubwa kwasababu watu wanaodaiwa kuwa ni Madalali wa shirika la nyumba la Taifa la NHC wamefika ofisini kwao asubuhi hii na kuanza kutoa vifaa vyao vyote nje ofisini.


Madalali wa NHC sasa wanatoa vitu nje kwenye ofisi za Mmiliki wa Tanzania Daima gazeti ambalo inahisiwa linamilikiwa na mh Mbowe.

Nadhani mtakumbuka siku kadhaa zilizopita mkurugenzi wa NHC ndugu Nehemia Mchechu alimtaja Mbowe kama miongoni mwa wadaiwa sugu wa shirika hilo na kudai alishamuandikia notisi yakulipa deni notisi ambayo imeisha jana.