Nafasi 594 za Kazi Kiwanda Cha Dangote ,Jinsi ya kuomba kazi soma hapa

NAFASI ZA KAZI DANGOTE CEMENT KUMBU NO;DIL/A00/2016/01

Kiwanda cha kuzalisha saruji cha DANGOTE Tanzania kilichopo mkoani Mtwara kilomita 23 barabara ya Lindi, Kata ya Mayanga, Kijiji cha HIARI, kinaalika maombi ya nafasi za kazi za madereva wenye uzoefu wa magari makubwa ya mizigo yasio pungua uzito wa tani 33 na urefu usiopungua mita 18


DEREVA GARI ZA MIZIGO NAFASI 594

SIFA ZA MWOMBAJI

I. Awe na umri wa miaka 26 hadi 55

II. Awe na lesini halali ya daraja E na mwenye uzoefu usiopungua miaka mi 5 ya kuendesha magari makubwa ya mizigo uzoefu wa kuendesha maroli wenye urefu usiopungua mita 18

III. Uzoefu usiopungua miaka mi 5 kwenye magari ya kuvuta tela

IV. Ajue kuandika taarifa na uzoefu wa kuweka kumbu kumbu zake kwa ufasaha

V. Awe na afya njema, akili timamu, ari ya kufanya kazi kwa tija, mwadilifu, mbunifu awezaye kujisimamia mwenyewe, katika kutimiza majukumu atakayo pewa

VI. Awe na wadhamini wanaoaminika na awe tayari kuchukuliwa alama za vidole

VII. Awe na uelewa wa kusoma na kuandika na kusikia Kiswahili na kingereza kwa uufasaha muhitimu wa kidato cha IV/VI

VIII. Awe mtumiaji mzuri wa muda katika safari atakazo pangiwa ndani na nje ya nchi

IX. Awe na uwezo mzuri wa kupaki garikwene nafasi zinazo bana

X. Awe na uwezo wa kusoma kiongoza ramani


VIAMBATANISHO

- Barua ya maombi ichapishwe au iandikwe kwa mkono

- Picha 2 za rangi zilizobanwa na vizuri katka barua ya maombi

- Vyeti vya mafunzo VETA/NIT pamoja na taaluma

- Cheti au barua kutoka muajiri wa sasa au aliyepita

- Barua toka kwa wadhamini wa 2 wanaoaminika zikiambatana na picha zao

- Cheti cha afya kutoka hospitali inayotambulika na serikali

- Cheti za kuzaliwa

MSHAHARA KWA MWEZI

DILSS Faraja lla 2 ngazi ya 3


NAMNA YA KUWASILISHA MAOMBI

- Andika nafasi unayoomba upande wa juu kulia mwa bahasha sambamba na kumbu kumbu namba ya tangazo

- Pamoja na maelezo ya uombaji onyoesha chanzo cha taarifa ya uombaji

- Maombi yatumwe kwa njia ya posta kupitia anuani zilizopo hapo chini

- Barua za mkononi hazitapokelewa

- Barua zote zitumwe kwa

MKUU WA IDARA YA RASILIMALI WATU NA UTAWALA,

DANGOTE INDUSTRIES LIMITED TANZANIA,

S.L.P 1241,

MTWARA