MAAJABU YA TENDO LA NDOA..!!

MAAJABU YA TENDO LA NDOA..!!
Kuna tofauti kubwa baina ya mwanamke na mwanaume wanapokuwa katika tendo la ndoa.
MWANAMKE:
1) Aibu huongezeka
2) Nguvu za mwili humuishia na mwili hulegea
3) Uwezo wa kufikiria huongezeka na kufika (to themaximum)
MWANAUME:
1) Aibu hutoweka kabisa
2) Nguvu za mwili huongezeka
3) Uwezo wa kufikiria(IQ) hushuka na kufikia zero! (hasa anapokuwa kileleni).
Katika hayo kuna mambo
tunajifunza:
a) Kumbe ndio maana vitabu vya mungu vinasema (mwanamume) aziniye na mwanamke hana akili kabisa; kwa
sababu kimaumbile na kisaikolojia uwezo wa kufikiri hutoweka!
b) Kama mwanamke anakuwa na uwezo mkubwa wa kufikiria (to the maximum) na mwanamume akili
na uwezo wa kufikiria vinashuka (to zero), bila shaka unaweza ukatambua kwa nini Samson “asingesalimika” kwa namna yeyote ile mbele ya Delila!
Nadhani wanaume tunapata somo letu
hapa;
“Mwanamke unaempa mwili wako kupitia tendo la ndoa, ikiwa ana nia mbaya ni rahisi mno kukumaliza kiulaiiiiiiiiiiiniiiiiiii”. Katikati ya tendo hili (akili yako inapokuwa sifuri) unaweza
kujikuta unakabidhi mshahara wote!
Unaweza kujikuta unaahidi kumnunulia gari wakati hata pikipiki imekushinda!
Unaweza kuikana familia yako mchana kweupe!
Na asikwambie mtu;
“Ahadi unazozitoa katikati ya tendo hili zina nguvu kubwa kuanzia ulimwengu wa roho hadi katika fikra.
Ndio maana ukidakwa na ukajikuta
umeropoka ahadi, ujue huo ni msala na hilo litakuganda mpaka ujute!”.
Pengine la muhimu (kwa wote) ni kujitahidi kuheshimu miili yetu na inapotolewa kutumika basi iwe ni “sadaka ya amani na haki” kwa wale wa halali na wanaostahili.