UCHAMBUZI KUELEKEA MCHEZO WA LIVERPOOL NA MANCHESTER UNITED

1. KIUNGO.
Liverpool wanaweza kuwakosa Wijnaldum na Lallana ambao wameweza kuwapa uwiano mkubwa kwenye kiungo. Sidhani kama Klopp ataingiza wachezaji wapya wawili kikosini ila kuna uwezekano Coutinho akarejea katikati na Emre Can kuongezeka. Mourinho anatakiwa kutumia nafasi hii kuwanyima raha Liverpool hasa kabla hawajatulia katikati mwa uwanja. Pogba akicheza mbele kidogo umbo lake una ubunifu vinaweza kumfanya Henderson akose ubora wa kukimbia uwanjani na mpira. Hiki ndicho Mourinho anatakiwa kuhakikisha kinatokea ili aweze kutoka salama Anfield. .



2. FALSAFA
Hii inaweza kuwa mara ya kwanza msimu huu ambapo Manchester United itaukana mpira. Mourinho anajua kuwa Liverpool wanapenda kupress na ili wakupress watataka uwe na mpira. Sasa Mourinho anatakiwa kukaa nyuma huku akitumia wachezaji warefu kupokea mipira mirefu kwa ajili ya counter attacks huku pia akijitahidi kila nafasi ya mipira ya adhabu na kona anaitumia. Liverpool wataendelea kutaka kuadhibu kupitia mnyumbuliko wa Coutinho, Firmino na Mane na hapa ndipo ambapo Mourinho atahitaji presha ya hawa itulizwe na kiungo mmoja ambaye hatokuwa na tamaa ya kwenda mbele. Herrera anaweza kutenda haki bahati nzuri anajua kutumia mpira mguuni.
.
3. FALSE 9 VS CENTRE FORWARD. 

Inawezekana Liverpool wakaendelea kutumia mfumo wa false 9 kupitia kwa Firmino. Huyu ana advantage mbele ya mabeki wa United kwa sababu kutokana na kupress vyema atawafanya wasiwe huru na mpira lakini pia kutokutulia kwake eneo moja kutafanya eneo la ulinzi lisiwe limetulia. Kwa Upande wa United watakuwa na Zlatan Ibrahimovic ambaye ni Center forward mzuri na ambaye ana nafasi ya kuwadhuru Liverpool kwa kupitia mipira ya juu. Liverpool hawapo vyema juu na hili Mourinho atahitaji Ibrahimovic awe vyema huku ikiwezekana kabisa Lovren akapewa kazi maalumu.
.

4. Udhaifu wa Liverpool ni zonal marking yao ambayo wachezaji wa United wakitumia counter vyema watapata kitu.
.
5. Udhaifu wa United upo kwenye kiungo. Hawajatulia hapa na Liverpool wana kasi zaidi eneo hili kuliko klabu nyingine yoyote. United wasipotulia wataumia. Liverpool inafunga sana kupitia viungo. .

Nicasius Coutinho Agwanda