NGUZO ZINAZOMJENGA MWANAUME

Kama kichwa kinavyojieleza hapo, siku hizi watu wamejikuta wakichanganyikiwa kutokana na mabadiliko ya kimila na kiutamaduni.

Zamani mtu ulikuwa ukifanya au ukiwa na tabia fulani basi utasikia wazazi wakikuambia hiyo sio tabia ya kike au ya kiume.

Duniani kila jambo huwa na sifa zake halikadhalika tabia.

Naomba wakina Mama ambao wanawatoto wakiume wachukue wajibu wa kuwafundisha watoto tabia zao na sifa zao.
Nguzo zinazomjenga Mwanaume halis

1. Ujasiri
Mwanaume halisi hawezi kuwa muoga kwani hulka ya mwanaume. Mwanaume sharti Awe jasiri ili aweze kuziba pengo la uwoga wa mwanamke kwani kihulka mwanamke ni muoga ukilinganisha na mwanaume.

2. Busara na hekima.
Mwanaume hapaswi kutoa maamuzi ya kukurupuka wala kutoa hukumu isiyo na haki. Mwanaume halisi huwa na Busara na Hekima katika maamuzi na mazungumzo.

3. Msimamo.
Mwanaume hapaswi kuyumbishwa hata Kama kakosea. Siku zote mwanaume hupaswa kuamini kuwa kile anachokifanya ni sahihi. Hivyo asifanye mambo kwa mashaka mashaka.
Pia aamini kuwa Mwanaume hakosei.

4. Akili na maarifa.
Mwanaume alipewa Tunu zote na Mungu, ili aweze kumfanya awe mfano wake. Mwanaume hupaswa kutenda kwa akili pasipo mihemko yoyote.
Mwanaume huongozwa na Akili na si kuongozwa na Moyo. Wanaume wengi walioanguka katika ulimwengu huu waliacha kutumia akili ambayo ni miongoni mwa nguzo za mwanaume kamili.

5. Sauti ya Mamlaka
Mwanaume lazima awe na sauti ya kuumba jambo likawa. Akisema kitu kifanyike hufanyika na kinyume chake. Mwanaume hakupewa sauti nzito Kama urembo bali Kama nyenzo ya kutiisha na kuleta utisho.
Mwanaume anapobana sauti ifanane na sauti ya mwanamke huharibu sauti ya mamlaka ambayo humfanya aheshimike.
Mwanaume hapaswa kuongea kwa kujiamini kwa kile anachoongea. Hapaswi kuiga tabia za kishoga au kuelezea habari za kusikia.

6. Mjongeo na Mikao.
Mwanaume hupaswa kutembea kwa mwendo wa kujiamini, mamlaka, kujitukuza. Mwanaume hapaswi kutembea akijitingisha sehemu zake zenye ashki Kama kiuno na makalioni. Jambo hili hufanywa na wanawake.

Mwanaume hapaswi kukaa mikao ya kiumbea, hupaswa kukaa mikao ya ufahari na kujiamini. Sio kujibinua binua.

7. Ubishi.
Mwanaume lazima usikubali kushindwa. Ndio maana unapaswa kuwa na akili. Mwanaume lazima ujue kutetea kile unachokiamini na sio unabisha bila hoja.
Wanaume wasio wabishi huishia kunyanyaswa na wanaume wenzao kwa kupigwa au hata wake zao.
Mwanaume hapaswi kukubali kushindwa kwa lolote na hata Kama anaona atashindwa hapaswi kusema mbele za watu.
Hii huhusu hata suala la kutafuta maisha.

8. Mwanasanaa.
Mwanaume kamili lazima awe msanii. Kufanya drama kwa mwanaume ni nyenzo muhimi Sana, ucheshi, kuimba, uchoraji n.k. kwaajili ya kumfurahisha yule umpendae.
Mwanaume asipokuwa Msanii huweza kuachwa na mke wake hata Kama ni tajiri wakutupa.
Wanawake hupenda wanaume Wasanii yaani waimbaji, ma-king Drama, waongeaji kwa maneno ya mvuto, wacheshi n.k.
Jambo hili ni tofauti na kinadada hawajajaliwa sanaa Kama wanaume.

9. Kufanya mapenzi.
Mwanaume kamili lazima ajue iwe kwa kujifunza au laa kufanya Mapenzi.
Endapo hutaweza jambo hilo basi utakuwa umepungukiwa pakubwa Sana.
Wanawake huchukulia hicho Kama miongoni mwa vipimo vyao kukupima.

10. Kiongozi.
Sifa zote hapo juu humfanya mwanaume kuwa kiongozi kwa kuiongoza familia na dunia kwa ujumla.